Sunday, June 22, 2014
skendo za mhamisha mjini agnes masogange
Siku chache baada ya Agness Gerard
'Masogange' kukimbilia nchini Afrika Kusini
'Sauzi' kwa kile alichodai ni kutafuta maisha
mazuri, rafiki wake wa karibu
aliyejitambulisha kwa jina la Jenifer ameibuka
na kuweka kila kitu hadharani juu ya nini
kilichomkimbiza mrembo huyo
Jennifer alisema kuwa kilichomuondoa nchini
mrembo huyo ni vidole vya watu ambao
wamekuwa wakimnyooshea kila alipopita
kuhusiana na skendo ya kukamatwa na
madawa ya kulevya.
Akizungumza na mwanahabari wetu, Jennifer
alisema kuwa kitendo hicho kilikuwa
kikimkera na kumkosesha raha Masogange
hivyo akaona njia rahisi ya kuondokana na hilo
ni kuhama jiji kwa muda mpaka watanzania
watakapoisahau skendo hiyo ndipo atarudi.
''Si kweli kwamba Masogange ameamua
kwenda kuishi Afrika ya Kusini kwa kupenda,
bali vidole vya watu waliokuwa wanaoneshana
kila sehemu alipokuwa anapita kwani wengi
wanamfahamu na alivuma na skendo ya
kukamatwa na madawa ya kulevya Afrika
Kusini hali ambayo ilikuwa inamnyima raha na
kuona njia sahihi ni kuhama kwa muda
Tanzania.'' alisisitiza jennifer.
Muda mfupi kabla ya kuondoka nchini,
Masogange alisema kuwa ameamua kuhamia
huko ambako anahisi ndiko maisha yake yalipo
na mipango mingi ya kimaisha anafanikiwa
kuliko Bongo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment