Historia mpya imeandikwa kwenye mechi ya
mwisho ya hatua ya nane bora iliyozikutanisha
Uholanzi dhidi ya timu ya Costa Rica, ambayo
kwa mara ya kwanza imefanikiwa kucheza
hatua ya robo fainali ya kombe la dunia.
Mchezo huo uliomalizika hivi punde umetumia
zaidi ya dakika 120 ili kuamua timu ya kwenda
kuchuana na Argentina kwenye nusu fainali.
Dakika 90 za mchezo huo ziliisha kwa
matokeo ya sare tasa, na mpaka mpira
unakwenda dakika 30 za nyongeza na
kumalizika milango bado ikabaki migumu na
ikaamuliwa kwenda kwenye mikwaju ya penati.
Uholanzi ikiwa haijawahi kushinda kwenye
mikwaju ya penati katika mashindano ya
kombe la dunia, ikafanikiwa kushinda kwa
penati 4-2 dhidi ya Costa Rica.
Pia hii ni mara ya kwanza kwa Uholanzi
kushinda mechi yoyote ambayo imevuka
kwenda kwenye hatua ya dakika za nyongeza.
Kwa matokeo hayo sasa Argentina itakutana
na Holland jumatano usiku, wakati Brazil
ikukutana na Ujerumani jumatatu hii.

mwisho ya hatua ya nane bora iliyozikutanisha
Uholanzi dhidi ya timu ya Costa Rica, ambayo
kwa mara ya kwanza imefanikiwa kucheza
hatua ya robo fainali ya kombe la dunia.
Mchezo huo uliomalizika hivi punde umetumia
zaidi ya dakika 120 ili kuamua timu ya kwenda
kuchuana na Argentina kwenye nusu fainali.
Dakika 90 za mchezo huo ziliisha kwa
matokeo ya sare tasa, na mpaka mpira
unakwenda dakika 30 za nyongeza na
kumalizika milango bado ikabaki migumu na
ikaamuliwa kwenda kwenye mikwaju ya penati.
Uholanzi ikiwa haijawahi kushinda kwenye
mikwaju ya penati katika mashindano ya
kombe la dunia, ikafanikiwa kushinda kwa
penati 4-2 dhidi ya Costa Rica.
Pia hii ni mara ya kwanza kwa Uholanzi
kushinda mechi yoyote ambayo imevuka
kwenda kwenye hatua ya dakika za nyongeza.
Kwa matokeo hayo sasa Argentina itakutana
na Holland jumatano usiku, wakati Brazil
ikukutana na Ujerumani jumatatu hii.

No comments:
Post a Comment