
Ukizungumzia taifa ambalo limetoa mastar
kadhaa wa soka Duniani hutoacha kulitaja
Brazil hii ni kufuatia rekodi zake kadhaa
ambazo limewahi kujiwekea kwenye medali ya
soka duniani leo limeingia kwa headline tena
taifa hili.
Ni kuhusu mtoto mdogo amabye kwa
kumtazama anaweza kuwa na umri usiozidi
miaka 3,amekua ni miongoni kati ya
walioumizwa na taarifa za kidaktari
zinazomhusu mchezaji Neymar kuwa
hatocheza mechi nyingine za Kombe la Dunia.
Kama unakumbuka Neymar alipata majeraha
baada ya kuumia kwenye mechi iliyochezwa
kati ya Brazil na Colombia na katika mechi
hiyo Brazil ilifanikiwa kushinda goli 2-1 na
kufanikiwa kuingia nusu Fainali.
July 08 Brazil ambao kimsingi ndio wenyeji wa
mashindano haya ya kombe la dunia itacheza
na Ujeruman,mchezo utakaochezwa bila
Neymar katika mechi ya Nusu Fainali.

No comments:
Post a Comment