Mwanamuziki anayefanya vizuri katika
gemu Dayna Nyange amesambaza beat ya
wimbo wake mpya ambao tayari
ameshaurekodi kwa lengo la kuwapima
wasanii wezi wa beats za wenzao kama
wataufanyizia tena.....
Hatua ya Dayna imekuja kutokana na
malalamiko aliyowahi kuyatoa siku za
nyuma ya kuibiwa beat ya wimbo wa
Number One na msanii Diamond Plutnumz
baada ya kumsikilizisha beat hiyo na
kumtaka afanye naye collabo.....
"Safari hii nimeacha akili yangu na hisia
zangu zitawale katika kile ambacho nina
kiamini kuwa ni sahihi kwangu hasa
katika huu wimbo mpya, tayari
nimeurekodi lakini nimewasambazia beat ili
nione nani atakayethubutu kuiba kama
ilivyokuwa mwaka jana," alisema Dayna
ambaye hivi sasa inasemekana yupo
kimapenzi na mshiriki wa big brother,
Nando.
Licha ya Dayna kutomtaja Diamond moja
kwa moja katika mtego wake huo lakini
ukweli unabaki palepale kwamba aliwahi
kumshutumu mwanamuziki huyo pamoja
na prodyuza Sheddy Clever kwa wizi wa
beat na kesi yao ilifika hadi Basata na
Cosota

gemu Dayna Nyange amesambaza beat ya
wimbo wake mpya ambao tayari
ameshaurekodi kwa lengo la kuwapima
wasanii wezi wa beats za wenzao kama
wataufanyizia tena.....
Hatua ya Dayna imekuja kutokana na
malalamiko aliyowahi kuyatoa siku za
nyuma ya kuibiwa beat ya wimbo wa
Number One na msanii Diamond Plutnumz
baada ya kumsikilizisha beat hiyo na
kumtaka afanye naye collabo.....
"Safari hii nimeacha akili yangu na hisia
zangu zitawale katika kile ambacho nina
kiamini kuwa ni sahihi kwangu hasa
katika huu wimbo mpya, tayari
nimeurekodi lakini nimewasambazia beat ili
nione nani atakayethubutu kuiba kama
ilivyokuwa mwaka jana," alisema Dayna
ambaye hivi sasa inasemekana yupo
kimapenzi na mshiriki wa big brother,
Nando.
Licha ya Dayna kutomtaja Diamond moja
kwa moja katika mtego wake huo lakini
ukweli unabaki palepale kwamba aliwahi
kumshutumu mwanamuziki huyo pamoja
na prodyuza Sheddy Clever kwa wizi wa
beat na kesi yao ilifika hadi Basata na
Cosota

No comments:
Post a Comment