MKONGWE wa Bongo Fleva, Godfrey Tumaini
‘Dudubaya’ anasakwa na polisi kwa RB namba
OB/RB/11650/2014 KUTISHIA KUUA mganga
wa jadi Mery Kapalisya ambaye inadaiwa
alikuwa akiishi naye kama mkewe.
Akisimulia mkasa mzima, Mery alisema
Dudubaya alitishia kumuua mara baada ya
kumfukuza katika nyumba waliyokuwa wakiishi
pamoja maeneo ya Tandale, jijini Dar.
“Mimi na Dudu (Dudubaya) tulikutana baada
ya kukutanishwa na Mabovu (msanii) ndipo
tukaanzisha uhusiano wa kimapenzi baada ya
kuniomba niwe naye na kunieleza matatizo
yake.
“Kwa sababu nilimpenda niliamua kumkubalia
na kuanza naye maisha ambapo tulikuwa
tukilala katika baa yangu nyumbani kwa akina
Mabovu.
“Tukiwa ndani ya uhusiano, Dudubaya alianza
kunibembeleza kwamba baa ile tuipe jina la
Mamba ikiwa ni chata yake, kwa sababu
nilimpenda niliamua kumkubalia lakini
nilimwambia aongeze herufi nyingine mbili
ambazo zitamaanisha na mimi nahusika,
tukakubaliana,” alisema Mery na kuongeza:
“Baada ya baa kubadilishwa jina, matatizo
yakaanza taratibu kwani walijaa wasanii wa
kila aina, baa ikaanza kuwa na sifa mbaya
mpaka wateja wote wakaondoka wale
waliokuwa wanajiheshimu.
”
Mery alisema alikuwa akimuonya Dudubaya
juu ya tabia za kumsaliti na kulala na
wanawake ndani ya nyumba pale anapokuwa
amesafiri kwenda kwenye mambo ya kitabibu
lakini alikuwa hasikii.
“Baada ya kunifukuza nyumbani, amenitumia
maneno mazito sana ambayo siwezi kusimulia
kiukweli lakini ninao ushahidi wa SMS,”
alisema Mery alipokuwa katika Kituo cha Polisi
Oysterbay.
Wakati Mery alipokuwa kituoni hapo, polisi
walimpigia simu Dudubaya, akasikiliza maelezo
ya polisi kisha akakata simu na alipopigiwa
tena, hakupokea.


‘Dudubaya’ anasakwa na polisi kwa RB namba
OB/RB/11650/2014 KUTISHIA KUUA mganga
wa jadi Mery Kapalisya ambaye inadaiwa
alikuwa akiishi naye kama mkewe.
Akisimulia mkasa mzima, Mery alisema
Dudubaya alitishia kumuua mara baada ya
kumfukuza katika nyumba waliyokuwa wakiishi
pamoja maeneo ya Tandale, jijini Dar.
“Mimi na Dudu (Dudubaya) tulikutana baada
ya kukutanishwa na Mabovu (msanii) ndipo
tukaanzisha uhusiano wa kimapenzi baada ya
kuniomba niwe naye na kunieleza matatizo
yake.
“Kwa sababu nilimpenda niliamua kumkubalia
na kuanza naye maisha ambapo tulikuwa
tukilala katika baa yangu nyumbani kwa akina
Mabovu.
“Tukiwa ndani ya uhusiano, Dudubaya alianza
kunibembeleza kwamba baa ile tuipe jina la
Mamba ikiwa ni chata yake, kwa sababu
nilimpenda niliamua kumkubalia lakini
nilimwambia aongeze herufi nyingine mbili
ambazo zitamaanisha na mimi nahusika,
tukakubaliana,” alisema Mery na kuongeza:
“Baada ya baa kubadilishwa jina, matatizo
yakaanza taratibu kwani walijaa wasanii wa
kila aina, baa ikaanza kuwa na sifa mbaya
mpaka wateja wote wakaondoka wale
waliokuwa wanajiheshimu.
”
Mery alisema alikuwa akimuonya Dudubaya
juu ya tabia za kumsaliti na kulala na
wanawake ndani ya nyumba pale anapokuwa
amesafiri kwenda kwenye mambo ya kitabibu
lakini alikuwa hasikii.
“Baada ya kunifukuza nyumbani, amenitumia
maneno mazito sana ambayo siwezi kusimulia
kiukweli lakini ninao ushahidi wa SMS,”
alisema Mery alipokuwa katika Kituo cha Polisi
Oysterbay.
Wakati Mery alipokuwa kituoni hapo, polisi
walimpigia simu Dudubaya, akasikiliza maelezo
ya polisi kisha akakata simu na alipopigiwa
tena, hakupokea.


No comments:
Post a Comment