Friday, July 4, 2014

Wema sepetu aomba msadaa TCRA kumsaka mtu alie tengeneza picha chafu ya mama yake mzazi

Miss Tanzania 2006/2007 Wema Sepetu
ameiomba Wizara ya Sayansi na Teknolojia
kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
( TCRA ) kumsaka mtu aliyetengeneza
picha chafu ya mama yake mzazi,
Mariam Sepetu na kisha kuisambaza
kwenye mitandao ya kijamii......

Akizungumza na mwanahabari wetu, Wema
alisema anaamini kuwa TCRA wanao
uwezo wa kumbaini mtu huyo ambaye
bado hajamfahamu ili sheria iweze
kuchukua mkondo wake kwani
amemdhalilisha mzazi wake bila sababu
yoyote....

"Nafanya utaratibu wa kwenda TCRA ili
wamsake aliyefanya kitendo hicho kwani
uwezo huo wanao,"

alisema Wema
Mrembo huyo alisema serikali isisubiri
mpaka tukio hilo limkute kiongozi wa
serikali ndo waanze kuhaha kwani tabia
hiyo inaonekana kuota mizizi baada ya
hivi karibuni kufanyiwa hivyo wabunge.


No comments:

Post a Comment

Total Pageviews