Mwili wa Kaimu Balozi wa Libya nchini, Ismail
Nwairat (39), umesafirishwa jana kwenda Libya
na shirika la ndege ya nchi hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa za awali kutoka Ofisi ya
Mawasiliano ya Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa, mwili wa balozi
huyo anayedaiwa kujiua kwa risasi Jumanne
wiki hii mchana akiwa ofisini kwake, mwili
wake utapokewa na ndugu zake.
Na kwamba taarifa zaidi juu ya maziko ya
balozi huyo zitatolewa na ndugu zake baada
kuupokea mwili huo nchini Libya.
Awali Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Dar
es Salaam, Suleiman Kova alisema uchunguzi
wa kifo cha kaimu balozi huyo umeanza na
kwamba watachunguza sababu za kujiua.
Kwa mujibu wa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha
Mawasiliano cha wizara hiyo, Mkumbwa Ally,
tukio hilo limeshtua Tanzania kwa kuwa si
jambo la kawaida kwa mwanadiplomasia
kujiua..

Nwairat (39), umesafirishwa jana kwenda Libya
na shirika la ndege ya nchi hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa za awali kutoka Ofisi ya
Mawasiliano ya Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa, mwili wa balozi
huyo anayedaiwa kujiua kwa risasi Jumanne
wiki hii mchana akiwa ofisini kwake, mwili
wake utapokewa na ndugu zake.
Na kwamba taarifa zaidi juu ya maziko ya
balozi huyo zitatolewa na ndugu zake baada
kuupokea mwili huo nchini Libya.
Awali Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Dar
es Salaam, Suleiman Kova alisema uchunguzi
wa kifo cha kaimu balozi huyo umeanza na
kwamba watachunguza sababu za kujiua.
Kwa mujibu wa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha
Mawasiliano cha wizara hiyo, Mkumbwa Ally,
tukio hilo limeshtua Tanzania kwa kuwa si
jambo la kawaida kwa mwanadiplomasia
kujiua..

No comments:
Post a Comment