Kama ilivyotokea kwa msanii nyota wa
kike wa bongo fleva, Rehema Chalamira
'Ray C' kuingizwa katika matumizi ya dawa
ya kulevya na mtu ambaye alitokea
kumwamini sana, ndivyo ilivyotokea sasa
kwa msanii anayefuata nyendo zake,
Winfrida Josephat 'Rachel' ambapo
anadaiwa kuvutishwa unga bila kujua....
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha karibu
na msanii huyo,Rachel amewekewa dawa
hizo kupitia kwenye bangi na wakati
mwingine kwenye sigara hivyo inakuwa
vigumu kubaini hila iliyofanyika....
Habari ambazo tumezipata zinadai kwamba
msanii wa kiume nyota wa bongo fleva
ambaye amewahi kutuhumiwa kutumia
dawa za kulevya ndiye anayemtengenezea
kokuteli hiyo inayotarajiwa kumwangamiza
siku za usoni....
"Huyu mtoto ameshaanza kutumia dawa
za kulevya.Huwezi amini, hata Ray C
ameshapewa taarifa, hivyo anamsaka
kuhakikisha anamtoa katika kifungo
alichojiingiza...
"Unajua Ray C anampenda sana kutokana
na namna anavyopenda kujiweka kama
yeye na hata jinsi anavyoimba nyimbo
zake, hivyo aliposikia madai hayo alianza
kumsaka kila kona lakini bado
hajafanikiwa kwani Rachel anamkimbia,"
kimesema chanzo hicho.
Hata hivyo habari zaidi zinasema kuwa
kutokana na namna Rachel anavyomuamini
msanii huyo wa kiume hajakubali kama
anachanganyiwa dawa za kulevya kwenye
bangi na sigara.
"Mwenyewe anajiona yupo sawa, lakini sisi
tunaona tofauti, hakika Rachel anapotea na
sijui nani atamuokoa.
"Tumeshamwabia kwamba anapotea lakini
haamini, tunaweza kusema kwamba Ray C
aliponea bahati, sasa sijui kama na yeye
atapata bahati kama alivyopata mwenzake,
" kilisema chanzo hicho
Rachel ambaye anatamba na wimbo wa
'upepo' hakuweza kupatikana kuzungumzia
tuhuma hizo

kike wa bongo fleva, Rehema Chalamira
'Ray C' kuingizwa katika matumizi ya dawa
ya kulevya na mtu ambaye alitokea
kumwamini sana, ndivyo ilivyotokea sasa
kwa msanii anayefuata nyendo zake,
Winfrida Josephat 'Rachel' ambapo
anadaiwa kuvutishwa unga bila kujua....
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha karibu
na msanii huyo,Rachel amewekewa dawa
hizo kupitia kwenye bangi na wakati
mwingine kwenye sigara hivyo inakuwa
vigumu kubaini hila iliyofanyika....
Habari ambazo tumezipata zinadai kwamba
msanii wa kiume nyota wa bongo fleva
ambaye amewahi kutuhumiwa kutumia
dawa za kulevya ndiye anayemtengenezea
kokuteli hiyo inayotarajiwa kumwangamiza
siku za usoni....
"Huyu mtoto ameshaanza kutumia dawa
za kulevya.Huwezi amini, hata Ray C
ameshapewa taarifa, hivyo anamsaka
kuhakikisha anamtoa katika kifungo
alichojiingiza...
"Unajua Ray C anampenda sana kutokana
na namna anavyopenda kujiweka kama
yeye na hata jinsi anavyoimba nyimbo
zake, hivyo aliposikia madai hayo alianza
kumsaka kila kona lakini bado
hajafanikiwa kwani Rachel anamkimbia,"
kimesema chanzo hicho.
Hata hivyo habari zaidi zinasema kuwa
kutokana na namna Rachel anavyomuamini
msanii huyo wa kiume hajakubali kama
anachanganyiwa dawa za kulevya kwenye
bangi na sigara.
"Mwenyewe anajiona yupo sawa, lakini sisi
tunaona tofauti, hakika Rachel anapotea na
sijui nani atamuokoa.
"Tumeshamwabia kwamba anapotea lakini
haamini, tunaweza kusema kwamba Ray C
aliponea bahati, sasa sijui kama na yeye
atapata bahati kama alivyopata mwenzake,
" kilisema chanzo hicho
Rachel ambaye anatamba na wimbo wa
'upepo' hakuweza kupatikana kuzungumzia
tuhuma hizo

No comments:
Post a Comment