
Rais Jakaya Mrisho Kikwete jana Jumapili Julai
6, 2014 alitembelea kwa mara ya pili
maonesho ya kimataifa ya bishara katika
viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya
Kilwa jijini Dar es salaam, baada ya ratiba yake
kutokamilika katika ziara yake aliyoifanya siku
ya Jumamosi kutokana na muda.
Na kama ilivyo ada wananchi walifurahi kuwa
naye karibu kama ambavyo yeye pia alifurahi
kujumuika nao kwenye maonesho hayo ya kila
mwaka.
Watoto ndio waliokuwa wakimvutia zaidi Rais
Kikwete ambapo kila mara alisimama na
kuwasalimia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na
baadhi ya wananchi waliotembelea maonyesho
ya Sabasaba.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiteta na watoto
aliokutana nao Sabasaba.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwaaga wananchi
mara baada ya kujumuika nao pamoja kwenye
Maonyesho ya Sabasaba jijini Dar.



No comments:
Post a Comment